Friday, October 21, 2016

Angel:Nitawapa kipaumbele watoto wa kike


Na: HADIJA ABDALLAH

Dar es salaam, Katibu mkuu wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha uandishi wa habari dar es salaam(DSJ)Angel william amehaidi kuweka usawa wa kijinsia kati ya wanafunzi wa kike na kiume chuoni hapo,ili kumpa nafasi mtoto wa kike kwenye  sekta mbali mbali chuoni hapo
Akizungumza na waandishi wa habari,katika maandimisho ya siku ya mtoto wa kike duniani yaliyofanyika octoba 11 mwaka huu chuoni hapo,angel amesema atahakikisha anaweka usawa  hasa kwa wanafunzi wa kike ili kuwapa fursa mbali mbali  na kuondoa mitazamo hasi iliyojengeka kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla
Amesema jamii inapaswa kutambua kitendo cha kumnyima nafasi mtoto wa
kike katika kufanya maamuzi ni kumnyima haki ya kijinsia,hivyo amewataka wanafuzi wa kike chuoni hapo kujitokeza kwenye fursa mbali mbali ili kuondoa dhana potofu zilizojengeka kwa watoto wa kike
Pia amesisitiza kauli mbiu ya mtoto kike  akiwezeshwa anaweza,Mara nyingi watoto wa kike wanadharauliwa kwa kuonekana hawana kitu katika jamii kwahiyo amesisitiza kuitumia kauli hiyo ili aweze kuhutumia fursa hiyo kuweka usawa baina ya mtoto wa kike na  wa kiume katika usawa wa kijinsia.
Aidha,Ameongeza kwa kusema kuwa uongozi wa serikali yake itawapa kipaumbele watoto wa kike ili kutoa fursa kubwa ya uongozi chuoni hapo kwani hiyo itapelekea watoto wa kike kujiamini kwa kila jambo ambalo watakalo lifanyahata pale watakapo maliza taaluma zao.
“Mtoto wa kike ana haki sawa na mtoto wa kiume katika kufanya maamuzi mbalimbali ,hivyo jamii inapaswa kuondoa dhana potofu ya kuwa msichana ni wa kufanya kazi za nyumbani ,kwani fikra hizo zinapaswa kuondolewa, nikiwa katibu mkuu wa serikali ya wanafunzi(DASJOSO) nahaadi nitawapa kipaumbele katika uongozi.Alisema Willium
Doreen Alex ambaye ni mwanafunzi wa stashahada ya kwanza chuoni hapo amesema,Amepokea vizuri siku ya mtoto wa kike duniani anaona kama faraja kubwa kwa maadhimisho ya siku hii ya leo kwani inamthamini na kumpa nafasi mtoto wa kike.
Amesema ,Kupitia siku hii atahakikisha anaonesha mfano kwa jamii kuwa msichana anaweza kama mvulana, endapo  atasikilizwa na kupewa nafasi kwenye sekta mbalimbali kwani hiyo itapelekea kufanya mambo makubwa tofauti na jamii inavyofikiri.
Aidha,Ameongeza kuwa serikali ya wanafunzi iwape kipaumbele watoto wa kike katika kuwapa nafasi za juu za uongozi chuoni hapo ili kuwapa morali na kujiamini katika kufanya maamuzi mbalimbali.
“Nimefurahi na nimepokea vizuri siku ya mtoto wa kike duniani nikiwa kama msichana natarajia kufanya mambo makubwa kwenye sekta mbalimbali ili kuondoa dhana potofu zilizojengeka katika jamii.”Alisema Alex
Mnamo mwaka 2012 umoja wa mataifa ulitangaza rasmi kuanza kuhadhimishwa kwa siku hii,Hivyo kila oktoba 11 ni siku ya mtoto wa kike duniani katika kutambua haki zao mbalimbali.Hivyo kwa Tanzania tunaadhimisha kwa miaka mitatu tangu kudhimishwa kwake.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni kuwezesha mtoto wa kike katika kufikia malengo ya maendeleo katika jamii na kumpatia fursa mbalimbali,Ili jamii itambue kuwa mtoto wa kike ana haki kama mtoto wa kiume.
Katika maadhimisho ya mtoto wa kike duniani,Katibu mkuu wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO) katika chuo cha uandishi wa habari Dar-es-salaam,Angel Willium ameelezea changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto wa kike chuoni hapo.
Hata hivyo,Katibu mkuu wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO) ameahidi kufanya mambo makubwa kwa watoto wa kike kupitia serikali yake,Ili kuwapa fursa zinazojitokeza katika chuo cha (DSJ) na ameitaka jamii kuondoa dhana potofu kwa mtoto wa kike kuonekana hawezi kuongoza kwenye ngazi za juu.






No comments:

Post a Comment