Friday, October 21, 2016

Nitaboresha michezo DSJ


Dar es salaam.Naibu waziri wa michezo wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO),Ally Makame amesema ataboresha michezo mbalimbali katika chuo hicho baada ya kuporomoka kwa takribani miaka miwili.
Akizungumza na waandishi wa habari chuoni hapo,Ally Makame amesema,Chuo cha DSJ hakina muhamko mkubwa katika sekta ya michezo tofauti na ilivyokuwa miaka mitatu nyuma,Kwasasa kimeshuka katika sekta hiyo ya michezo kutokana na wanafunzi kukosa morali katika kushiriki michezo.
Amesema,Ili kuweza kuboresha sekta ya michezo chuoni hapo,Tayari ameshakutana na makocha wa michezo mbalimbali ili kuzungumzia na kutatua changamoto hizo za michezo katika chuo cha (DSJ) kwa lengo la kurudisha ramani ya michezo chuoni hapo.
Pia amesema,Ili kukuza na kuboresha sekta ya michezo ameutaka uongozi wa juu chuoni hapo kushirikiana na uongozi wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO) ili kuimarisha zaidi sekta hiyo ya michezo pamoja na sekta nyinginezo chuoni hapo.
Aidha,Ameongeza kwa kushukuru uongozi wa chuo unapaswa kuweka mashindano ili kuweza kukuza sekta ya michezo pamoja na kupata timu imara nayenye ushindani na kuwasisitiza wachezaji wa chuo cha (DSJ) pindi mazoezi na sio kusubiria mpaka mechi ndipo wafanye mazoezi.
‘’Napenda kuwasisitiza wachezaji wa chuo chetu cha (DSJ) tusisubiri mpaka mechi ndipo tufanye mazoezi kwani jambo hili litapelekea kushuka kwa sekta ya michezo.”Alisema Makame
Hemedi Fikiri ambaye ni mwanafunzi wa stashahada ya kwanza chuoni hapo amesema,Anaamini Makame ataimudu sekta ya michezo chuoni hapo itakayopelekea kuleta mabadiliko makubwa na kuondoa matabaka yaliyopo katika sekta ya michezo chuoni hapo.
Amesema,Baadhi ya wanamichezo wameweka matabaka ya urafiki,Ikiwa kupanga timu bila kufuata kanuni na utaratibu za kimichezo na baadhi yake hupelekea sekta ya michezo kuporomoka chuoni,Pia amewashauri wachezaji wa chuo cha (DSJ) kuondoa chuki zisizokuwa na tija ili kuboresha sekta ya michezo.
“Ili kukuza sekta ya michezo chuoni kwetu lazima wachezaji waondoe chuki zisizokuwa na tija pamoja na kuondoa matabaka ya urafiki ili kusaidia sekta ya michezo chuoni kwetu.”Alisema Fikiri
Baada ya mchakato wa uteuzi wa baraza la mawaziri lililoteuliwa mnamo oktoba mosi mwaka huu,Mawaziri walitoa ahadi mbalimbali za utekelezaji katika majukumu lakini baadhi ya wanafunzi walisubiria ahadi ya Naibu waziri wa michezo hatasemaje katika sekta yake ya michezo baada ya kuteuliwa.
Naibu waziri wa michezo wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO),Ally Makame amehaidi kutatua changamoto mbalimbali katika sekta ya michezo ili kuimarisha hali na nguvu chuoni hapo,Na kutoa ubaguzi wa kimatabaka katika michezo ili tuweze kufika mbali kama ilivyokuwa miaka iliyopita.
Uongozi wa juu wa chuo cha uandishi wa habari Dar-es-salaam (DSJ) umehaidi kushirikiana bega kwa bega katika kuboresha sekta ya michezo chuoni hapo na kuwaandalia mashindano iliwaweze kujiweka sawa na kujianda kushindana na vyuo vingine na kuwaongezea vifaa vya michezo.
Naibu waziri wa michezo amesisitiza kwa wanamichezo kujitokeza kikamilifu katika kushiriki katika michezo mbalimbali na kujiweka na maandalizi ya mashindano yatakayokuja siku za usoni na kushiriki katika mechi za madarasa ilikutafuta timu itakayotuwakilisha.


No comments:

Post a Comment