JINSI YA KUTUNZA NGOZI YA USO
Uso unahitaji kutunzwa vizuri maana ndio reception ya mwili wako, matunzo ya uso hayaitaji vipodozi vya gharama ni ufuatiliaji wa vitu vidogo vidogo tu.
Osha uso wako na sabuni walau mara mbili kwa siku kuweweka katika hali ya usafi na kuondoa mafuta, vumbi, jasho nk
Usilale bila kuondoa makeup usoni maana ukifanya hivyo uwezekano wa kupata chunusi ni mkubwa sana na ngozi inachakaa haraka. Osha uso wako vizuri kuondoa makeup kabla ya kulala na kuiacha ngozi ipumue.
Unaponunua lotion, cream au sabuni hakikisha unanunua inayoendana na ngozi yako kama ni ngozi kavu au ya mafuta. Soma maelekezo kabla ya kununua, mfano sabuni au lotion zenye ndimu au limao mara nyingi ni za ngozi ya mafuta, zenye aloe vera au tango kwa ngozi zote.
Sugua uso wako na sabuni na kitaulo laini taratibu kisha unaosha walau mara moja kwa wiki kuondoa ngozi iliyokufa (dead skin) na kuiacha ngozi yako inangaa na laini. Kama ngozi yako ina mafuta mengi fanya hivyo mara mbili kwa wiki.
Ili kuwa na ngozi nyororo na inayovutia hakikisha pia una kunywa maji ya kutosha, pata usingizi wa kutosha, kula vizuri, epuka pombe kupita kiasi na sigara zitakuzeesha. Kila mtu anaweza kuwa na ngozi inayovutia.
Hapa nazungumzi matunzo ya uso ya kawaida sio kuondoa madoa na chunusi. Ukipenda kujua jinsi ya kuondoa chunusi kwa vitu asilia bonyeza Link usome, http://eunicemahundi.com/2015/02/03/jinsi-ya-kuondoa-chunusi-kwa-kutumia-vitu-asilia/
Uso unahitaji kutunzwa vizuri maana ndio reception ya mwili wako, matunzo ya uso hayaitaji vipodozi vya gharama ni ufuatiliaji wa vitu vidogo vidogo tu.

Osha uso wako na sabuni walau mara mbili kwa siku kuweweka katika hali ya usafi na kuondoa mafuta, vumbi, jasho nk

Usilale bila kuondoa makeup usoni maana ukifanya hivyo uwezekano wa kupata chunusi ni mkubwa sana na ngozi inachakaa haraka. Osha uso wako vizuri kuondoa makeup kabla ya kulala na kuiacha ngozi ipumue.

Unaponunua lotion, cream au sabuni hakikisha unanunua inayoendana na ngozi yako kama ni ngozi kavu au ya mafuta. Soma maelekezo kabla ya kununua, mfano sabuni au lotion zenye ndimu au limao mara nyingi ni za ngozi ya mafuta, zenye aloe vera au tango kwa ngozi zote.


Ili kuwa na ngozi nyororo na inayovutia hakikisha pia una kunywa maji ya kutosha, pata usingizi wa kutosha, kula vizuri, epuka pombe kupita kiasi na sigara zitakuzeesha. Kila mtu anaweza kuwa na ngozi inayovutia.

Hapa nazungumzi matunzo ya uso ya kawaida sio kuondoa madoa na chunusi. Ukipenda kujua jinsi ya kuondoa chunusi kwa vitu asilia bonyeza Link usome, http://eunicemahundi.com/2015/02/03/jinsi-ya-kuondoa-chunusi-kwa-kutumia-vitu-asilia/
Jinsi ya kutumia Asali katika Urembo wa Nywele na Ngozi .
Jinsi ya kutumia Asali katika Ngozi
Asali hutumika kulainisha Ngozi
Asali ina asili ya kuvuta unyevu kutoka kwenye hewa na kuipa ngozi uwezo wa kuhifadhi unyevu hivyo ni faida kwa mtu mwenye ngozi kavu.
Jinsi ya kuandaa
Chukua asali mbichi kijiko kimoja cha chai kisha paka usoni, kaa nayo kwa dakika 15 hadi 20 kisha safisha uso wako.
Asali katika kusafisha ngozi, kutibu na kuzuia chunusi
Kutokana na uwezo wa asali katika kuua bacteria na kuvuta uchafu katika matundu ya ngozi asali itakusaidia kutatua tatizo la chunusi.
Jinsi ya Kuandaa
Chukua asali mbichi Kijiko kimoja cha chakula changanya na mafuta ya nazi vijiko viwili changanya mchanganyiko uwe mlaini kisha paka usoni huku ukisugua taratibu kwa kufanya kama viduara huku ukiepuka kufikisha machoni. ukimaliza kusugua uso na mchanganyiko wako osha uso wako.
Jinsi ya kuandaa kama kisafisha ngozi, exfoliator
Changanya kijiko kimoja asali na kijiko kimoja baking soda. tumia mchanganyiko huu kusugua ngozi yako. Asali inaongeza lishe na chembe chembe kuzuia madhara yanayotokana na sumu za hewani zinazozeesha ngozi. Baking soda inasaidia kusafisha matundu ya ngozi.
Asali inasaidia ngozi iliyoungua na jua kujirudi na kung'aa.
Jinsi ya kutumia asali katika nywele
Asali inatibu nywele kavu zilizopauka, na kulainisha ngozi kavu ya kichwa na kutibu muwasho kichwani.
Jinsi ya kufanya
Changanya kijiko kikubwa cha asali na maji ya uvuguvugu kisha paka kichwani Acha kwa muda wa saa 1 iwe kama conditioner kisha safisha nywele zako.
pia
Unaweza kuchanganya asali kiasi cha kijiko kimoja mpk viwili katika maji vikombe vitano kisha safishia nywele zako taratibu, yaani yapitishe tu hayo maji kwenye nywele zako ambazo ni safi.
Tahadhari: Asali kwa kiasi kikubwa hupausha weusi wa nywele kutokana na Hydrogen Peroxide inayopatikana ndani ya asali.
Ni vema ukatumia asali mbichi kujihakikishia faida za asali katika mwili wako.
Iwapo unavutiwa na matumizi ya kitu cha asili katika urembo wako unaweza kuongeza kitu hicho katika kitu kingine unachotumia mfano katika steaming yako au scrub unayotumia.
No comments:
Post a Comment